Friday, September 14, 2012

WAJASIRIMALI WALIOFUZU WAPEWA VYETI

 Dr Didas Lunyungu  akitoa cheti  cha kufuzu mafunzo ya Ujasiriamali kwa  wajasiriamali waliohudhuria semina iliyofanyika kwenye ukumbi wa Africenter Ilala jijini Dar es Salaam

 
Mafunzo ya Ujasiriamali yaliyokuwa  yakiendelea kwenye ukumbi wa Africenter Ilala jijini Dar, yanatarajiwa kukamilika  leo 
Akizungumza na mtandao huu Mkurugenzi wa kampuni ya Mjasiriamali Kwanza inayoendesha  semina hizo kubwa hapa nchini Dr Didas Lunyungu amesema kuwa amefanikiwa kutoa vyeti zaidi ya 1000 kwa wajasiriamali waliokuwa wakihudhuria mafunzo kwenye semina hizo baada ya kufaulu kwao vizuri na kuwa tayari kwa  kujitengenezea bidhaa majumbani mwao na kuuza kwa wateja ili kujiongezea kipato.

"Tumefanikiwa kutoa vyeti zaidi ya 1000 kwa wajasiriamali walifaulu vizuri mafunzo yao huu ni mwanzo wa harakati zetu kuwafanya watanzania  kuondokan ana woga wa ugumu wa maisha kwa kujitengenezea bidhaa ambazo watauza na baadae kujipatia fedha za kuendesha maisha"  alisema Didas.

0 COMMENTS:

Post a Comment