Monday, September 3, 2012

3500 WAHUDHURIA MAFUNZO DAR LIVE

WATU zaidi ya 3500 walijitokeza kupokea mafunzo ya Ujasiriamali kutoka kwa Mwalimu mwenye  uzoefu na mafanikio makubwa  kwenye kufundisha  masomo hayo Dr Didas Lunyungu, yaliyofanyika kwa siku nne mfululizo katika ukumbi maaraufu wa  Dar Live  uliopo Mbagala  jijini Dar Es Salaam.

Katika mafunzo hayo yaliyohudhuliwa  pia  na vyombo  mabalimbali vya habari nchini, wajasiriamali walijifunza kwa  vitendo kutengeneza  bidhaa mbalimbali za nyumbani na mashabani, zikiwemo sabuni za  kufulia, Batiki, na  vitu vingine  vingi.

Mmoja  ya wajasiriamali waliojitokeza katika  semina hiyo Bi Neema  Mussa aliuambia  mtandao huu kuwa kampuni ya  Mjasiriamali kwanza nchini ya Dr Didas  ni mkombozi mpya wa maisha ya Watanzania  wengi  ambayo yako kwenye hali tete  kutokana na  kukosekana kwa  uchumi imara hapa nchini.

"kwa  kweli kampuni hii  inafanya jambo jema  na kubwa  sana  ambalo linatukomboa wananchi wengi hivi sasa  kutoka  mdororo wa  kiuchumi tulionao kutokana na mafundisho bora  ya kutengeneza bidhaa  tunayaopata  tukiwa kwenye semina"  alisema. 

Akiendelea  zaidi  Bi Neema alitoa wito kwa serikali kuipa  nguvu kampuni hii  ili iweze kuwafikia watanzania wengi zaidi ambao  kwa hakika  wan awakati mgumu kimaisha  na kuwakomboa  kutoka  shida nyingi za  ukosefu wa fedha jambo linaweza kuharakisha  maendeleo miongoni mwao
Mmoja wa maelfu ya wajasiriamali, akifanya  maohjiano na mtangazaji wa  runinga ya Taifa TBC, wakati wa  semina  kubwa  iliyofanyika ndani ya DAR LIVE Mbagala jijini  Dar.
Maelfu ya wakazi wa jiji na wengine  kutoka  mikoa mbalimbali nchini wakitoka ndani ya ukumbi wa Dar Live  mara baada ya kumalizika kwa semina  ya ujasiriamali iliyokuwa  ikiongozwa na Mkurugenzi wa kampuni ya Mjasiriamalikwanza Dr Didas Lunyungu mwishoni mwa  wiki iliyopita. 

0 COMMENTS:

Post a Comment